Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Wabunge kuchukuliwa hatua Kisheria



Msajili Msaidizi wa vyama vya siasa nchini, Sisty Nyahonza amesema sheria inaruhusu kuchukua mkondo wake kwa Mbunge yoyote atakayezidisha kutumia gharama kubwa katika chaguzi mbalimbali, ambapo amesema gharama ya juu ni milioni 88.









Hayo amesema kupitia kipindi cha East Africa Breakfast cha East Africa Radio kuwa  sheria hiyo imeanza mchakato mwaka 2006 na kukamilika 2010, inasema mtu achaguliwe kutokana na uwezo wake wala sio pesa.

Gharama ya kuendesha kampeni za uchaguzi inatokana na ukubwa wa jimbo lenyewe lakini kuna kiwango maalumu ambacho taasisi imekipanga, kiwango cha chini kinaanzia milioni 33 huku kiwango cha juu ni milion 88.

''Kila jimbo lina kiwango chake , kama kiwango ambacho kimepangwa kikipita tunayo nguvu ya kuchunguza namna gani gharama kubwa imetumika ili muhusika achukuliwe hatua.

Alipoulizwa juu ya kujiridhisha kama kweli wagombea wametumia kiasi ambacho kimepangwa na taasisi hiyo amesema wana njia nyingi ikiwemo kushirikiana na Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

''Tuna njia nyingi za kufahamu kama tuna shaka na matumizi ya kuendesha kampeni zimezidi, tunashirikiana na Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa, tuna uwezo wa kufuata ripoti zote ambazo zimefanyika kupitia chama husika pamoja na kutafuta taarifa kwa wasamalia wema''.

Kwa uchaguzi ambao umefanyika mwaka 2015 kiwango cha chama cha siasa kimeruhusiwa kutumia kiasi cha bilion 17 kwa Rais, Wabunge na Madiwani.

Ambapo katika kampeni za Rais sheria inataka atumie shilingi bilioni 6 hadi mwisho wa uchaguzi, wakati madiwani wanaoishi mijini wametengewa milioni 8 huku wale wa vijijini watumie milion 6.

Katika sheria hiyo majimbo 267 ya Tanzania ambapo wabunge wanagombania wanatakiwa watumie kuanzia milioni 33 kiwango cha mwisho milioni 88 kisizidi zaidi ya hapo. Japo kuna majimbo yanaainishwa kabisa ambayo hayatakiwi kuvuka shilingi milioni 33.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...