Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Palestina yazika wahanga, yailaani Marekani

MTEULE THE BEST

Serikali ya Palestina imekataa wito wa Marekani kutaka sehemu ya Ukuta wa Magharibi katika Mji Mkongwe wa Jerusalem kubakia kwenye udhibiti wa Israel, huku maziko ya Wapalestina waliouawa kwenye maandamano wakizikwa

Gazastreifen BegrƤbnis nach Luftangriff (picture-alliance/Zumapress)
Afisa wa ngazi za juu kwenye serikali ya Palestina, Nabil Abu Rudeineh, ameliambia shirika la habari la WAFA kwamba kamwe Wapalestina hawatakubali mabadiliko yoyote kwenye mpaka wa 1967 wa Jerusalem Mashariki.
"Msimamo huu wa Marekani unathibitisha kwa mara nyengine kwamba utawala wa sasa wa nchi hiyo haupo kabisa kwenye suala la kupatikana amani na badala yake unataka kuuimarisha ukaliaji wa kimabavu," alisema.
Afisa mmoja wa ngazi za juu wa Marekani alisema kabla ya kuanza kwa ziara ya Makamu wa Rais Mike Pence kwenye mataifa ya Misri, Israel na Ujerumani, kwamba nchi hiyo haiwezi kuona "ni kwa namna gani Ukuta wa Magharibi usiwe sehemu ya Israel" hata ikiwa patakuwa na makubaliano baina ya Waisraeli na Wapalestina. 
Ukuta huu, ambao ni mabaki ya upande wa magharibi wa Hekalu la Pili, ni sehemu takatifu kwa Mayahudi wengi na ni sehemu ya eneo pana lililogeuka kiini cha mzozo wa kidini kwenye mji wa Jerusalem, likifahamika kama Mlima wa Hekalu kwa Mayahudi na Makaburi Matakatifu kwa Waislamu.
'Mashahidi' wazikwa
Maandamano makubwa yamekuwa yakifanyika kote Mashariki ya Kati kupinga uamuzi wa Rais Donald Trump wa Marekani.
Maandamano makubwa yamekuwa yakifanyika kote Mashariki ya Kati kupinga uamuzi wa Rais Donald Trump wa Marekani.
Haya yanatokea katika wakati ambapo Wapalestina wakiwazika wahanga wa hivi karibuni kabisa wa mashambulizi ya Israel dhidi ya waandamanaji wanaopinga tamko la Rais Donald Trump wa Marekani la kuitambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa taifa hilo la Kiyahudi.
Miongoni mwa watu wanne waliouawa jana (Ijumaa) na kuzikwa leo, ni kijana wa Kipalestina aliyekuwa amekatwa miguu katika mashambulizi ya Israel ya miaka tisa iliyopita. 
Ibrahim Abu Thuraya, aliyekuwa na miaka 29, aliuawa akiwa kwenye kigari chake cha magurudumu mawili jana kwenye Ukanda wa Gaza. Afisa mmoja wa jeshi la Israel alisema kuwa matukio kuhusika na mauaji ya Abu Thuraya yalikuwa yakichunguzwa, huku maafisa wa afya wa Palestina wakisema kijana huyo hakuwa kitisho chochote kwa jeshi la Israel.
Mataifa wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC) wameitambua Jerusalem Mashariki kuwa mji mkuu wa Palestina.
Mataifa wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC) wameitambua Jerusalem Mashariki kuwa mji mkuu wa Palestina.
Kwa wiki ya pili mfululizo, maeneo ya Ukingo wa Magharibi na Ukanda wa Gaza yamekumbwa na maandamano na machafuko, kufuatia tangazo la Trump na pia hatua ya kuagiza kuhamishwa kwa ubalozi wa nchi yake mjini Tel Aviv kwenda Jerusalem. Takribani ulimwengu mzima umelaani hatua hii, kasoro Marekani na Israel yenyewe.
Mataifa ya Kiislamu yaja juu
Katika kile kinachoonekana kama kulipiza kisasi, mataifa ya Kiislamu nayo yalitangaza kuitambua Jerusalem Mashariki kuwa mji mkuu wa Palestina kwenye mkutano wa dharura ulioitishwa na Uturuki wiki hii. 
Vile vile, kuna mipango ya kuifanya Palestina itambuliwe kama mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa, na huku Uturuki ikitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuulaani uamuzi wa Trump.
Vuguvugu la kijeshi la Hamas, ambalo linatawala Ukanda wa Gaza, limekuwa na msimamo mkali zaidi, likisema kwamba Jerusalem "ni mji wa Kiislamu na Kiarabu" na ikikataa muafaka wowote juu ya hilo.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...