Ruka hadi kwenye maudhui makuu

OIC yasema Jerusalem ni ya Palestina

MTEULE THE BEST

Viongozi wakuu wa mataifa wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC) wamesema wanaitambua Jerusalem kama mji wa Palestina na kwamba hawatakubali kuona hilo likibadilika, wakiitaka Marekani kufuta msimamo wake.
Wakikutana jijini Istanbul hivi leo (13 Disemba), viongozi wameitaka Marekani kufuta mara moja uamuzi wake wa kuutambua mji wa Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel, huku wakitishia kuchukuwa hatua kali dhidi ya Marekani na Israel endapo wataendelea na mipango yao ya kuufanya mji huo mtukufu kwa dini zote tatu - Ukritso, Uislamu na Uyahudi - kuwa makao makuu ya Israel.
Rais Mahmoud Abbas wa Palestina amewaambia viongozi wajumbe wa mkutano huo kwamba uamuzi wa Marekani kuitambua Jerusalem kama mji mkuu wa Israel ulikuwa uhalifu, akiifananisha na kitendo cha Donald Trump kuugawa mji huo kama vile ni sehemu ya Marekani. Na kwayo, amesema Abbas, serikali ya Marekani haiaminiki tena kwenye mazungumzo ya amani ya Mashariki ya Kati.
"Haitakubalika tena kwa Marekani kuwa na jukumu lolote kwenye mchakato wa kisiasa kwa sababu imejiegemeza upande mmoja wa Israel. Huo ndio msimamo wetu na tunataraji nanyi mutatuunga mkono."
Akiufungua mkutano huo, mwenyeji Rais Tayyip Erdogan wa Uturuki, alisema anabeba jukumu la kuitangaza rasmi Jerusalem kuwa mji mkuu wa dola la Palestina huku akitaka uungwaji mkono wa viongozi wengine wa Kiislamu duniani.
"Nazialika nchi zote ambazo zinalinda sheria ya kimataifa na haki, kuitambua Jerusalem kama mji mkuu wa dola la Palestina lililokaliwa kimabavu. Hatuwezi kuchelewesha hatua hii zaidi. Kama nchi za Kiislamu, hatutavunjika moyo kamwe kwenye madai yetu ya Palestina yenye mamlaka kamili na iliyo huru ambayo Jerusalem ni mji wake mkuu."

"Lazima Jerusalem isalie ya Waislamu"



Mwenyeji wa mkutano, Rais Tayyip Erdogan wa Uturuki, anataka Jerusalem itambuliwe rasmi kama mji mkuu wa Palestina.
Erdogan aliwaambia viongozi na mawaziri hao zaidi ya 50 wa mataifa ya Kiislamu kwamba uamuzi wa wiki iliyopita wa Trump ulikuwa zawadi kwa vitendo vya Israel, ukiwemo ukaliaji kimabavu, ujenzi wa makaazi ya walowezi, utwaaji wa ardhi na mauaji na ghasia zilizochupa mpaka.
Naye Rais Hassan Rouhani wa Iran alisema kuwa nchi yake iko tayari wakati wowote kusaidiana na mataifa mengine kuhakikisha uhuru wa Palestina unapatikana na kuurejesha nyuma ule aliouita ukorofi wa Israel na Marekani.
"Marekani haijawahi kuwa mpatanishi mkweli na kamwe haitakuwa. Kitendo hiki cha sasa kimelifanya hilo lionekane wazi kwa watu wote waliotarajia Marekani ingelikuwa na nia ya kutatua suala la Palestina. Kwamba Marekani inachotaka ni kupata maslahi makubwa zaidi kwa Mazayuni na haiheshimu matakwa halali ya Wapalestina."
Jerusalem, mji unaozingatiwa na Mayahudi, Wakristo na Waislamu kuwa mtukufu kwao, ni mahala ulipo msikiti wa tatu kwa utukufu kwa Waislamu na umekuwa kiini cha mzozo wa Israel na Palestina kwa miongo kadhaa sasa.
Israel iliitwaa sehemu ya mashariki ya mji huo kutoka kwa Waarabu mwaka 1967 na kisha kuifanya kuwa sehemu yake, kitendo ambacho kamwe hakijawahi kutambuliwa na 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...