Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mwanamke aliyemuua mume wake ili aishi na mpenzi wake India


Swati Reddy (kulia) na mpenzi wake wanadaiwa kumuua mume wake Sudhakar (kushoto) mwezi uliopita


Wapenzi wiwili nchini India wamekamatwa kwa kumuua mume wa mwanamke na kisha kujaribu kumfanyia upasuaji wa kubadilisha sura mwanamume mpenzi ili aweze kuchukua mahala pake,





Tindi kali ilimwagwa kwenye uso wa mwanamume, mpenzi wa mwanamkea, katika shambulizi lililopangwa, huku wapenzi hao wakipanga kusema kuwa sura yake ilikuwa imebadilika baada ya upasuaji.





Lakini ndugu wa bwana wa mwanamke aligundua mpango huo alipofika hospitalini.








Alitoa malalamiko yake kwa polisi ambao walifanya uchunguzi wa vidole na kugundua njama huyo.





Mke, Swati Reddy amekamatwa. Polisi waliiambia BBC kuwa watamkamata pia mpenzi wake, Rajesh Ajjakolu mara atakapotibiwa majeraha yake na kuruhusiwa kuondoka hospitalini.



Image captionRajesh Ajjakolu alilazwa hospitalini akiwa na majeraha ya uso

Bwana Sudhakar Reddy anadaiwa kuuliwa usiku wa tarehe 26 Novemba na mwili wake kutupwa siku iliyofuatia. Hadi sasa mwiwi huo bado haujapatikana.





Polisi wanasema kuwa mwanamke huyo amekiri kuwa walimuua mume wake.





Rajeshi Ajjakolu alilazwa hospitalini tarehe 28 Novemba huku Bi Reddy akiwajulisha familia ya mume wake kuhusu shambulizi la tindi kali.








Polisi wanasema kuwa wazazi wa Bw. Reddy waliamini kuwa mwanamume ambaye alikuwa akipata matibabu alikuwa ni mtoto wao na kulipa hadi dola 7,758 kama bili ya hospitali.





Njama hiyo haikugunduliwa hadi tarehe 9 mwezi Disemba, wakati ndugu yake Reddy, alifika hospitalini humo na kuwajulisha polisi aliposhuku kuwa mwanamume huyo hakuwa ndugu yake.




Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...