Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tanzania yajitenga na Trump kuhusu Jerusalem

MTEULE THE BEST

Religious sites in Jerusalem's Old City
Mji wa Jerusalem una maeneo matakatifu kwa Waislamu, Wakristo na Wayahudi
Tanzania imesema haikubaliani na hatua ya Rais wa Marekani Donald Trump ya kuutambua mji wa Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.
Wizara ya mambo ya nje ya Tanzania kupitia taarifa imesema nchi hiyo inaunga mkono makubaliano ya kimataifa ambayo yanatambua haki ya watu wa Palestina kumiliki Mashariki mwa Jerusalem kama ilivyokuwa kwenye mpaka wa kabla ya mwaka 1967.
"Tanzania inaunga mkono msimamo wa Umoja wa Mataifa wa suluhu ya mataifa mawili ambayo unatoa nafasi ya Israel na Palestina kuwepo kwa pamoja zikiwa na mipaka salama," taarifa hiyo iliyotuwa saini na Waziri Augustine Mahiga imesema.
Bw Trump kando na kuitambua Jerusalem kama mji mkuu wa Israel, alisema nchi hiyo pia itahamisha ubalozi wake kutoka Tel Aviv.
Bw Mahiga amesema ubalozi wa Tanzania utaendelea kuwepo mjini Tel Aviv.
Msimamo wa Tanzania unaenda sambamba na msimamo wa mataifa mengi ya Afrika pamoja na Tume ya Umoja wa Afrika (AU).
      Mwenyekiti wa tume hiyo Moussa Faki alikuwa ametahadharisha kwamba hatua ya Trump "itaongeza uhasama kanda hiyo na hata maeneo mengine na kutoa changamoto zaidi katika juhudi za kutafuta suluhu ya mzozo wa Israel na Wapalestina.
      Alisema Umoja wa Afrika unaendelea kuwaunga mkono Wapalestina na juhudi zao za "haki za kuwa na taifa huru ambalo litakuwa na Jerusalem Mashariki kama mji wake mkuu."
      "Hatua hii inatishia sio tu Mashariki ya Kati bali pia inachokoza ulimwengu woye wa Waislamu. Tunahofia kwamba hatua hii haitaathiri sio tu Afrika vibaya, bali pia itaifanya hali, ambayo kwa sasa inahitaji suluhu ya maiafa mawili, kuwa mbaya zaidi kuliko awali," alisema Bw Faki.
      Jumatano, mataifa 57 ya Kiislamu yalitoa wito kwa Jerusalem Mashariki kutambuliwa kama mji mkuu wa Wapalestina.
      Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan alikuwa ameyahimiza mataifa hayo katika mkutano mkuu wa muungano wa nchi za Kiislamu (OIC), kufanya hivyo akisema hatua ya Marekani ya kuutambua mji huo kama mji mkuu wa Israel ni "batili".
      Bw Erdogan pia kwa mara nyingine aliishutumu Israel na kuiita "taifa la kigaidi".
      KIongozi wa Wapalestina Mahmoud Abbas amesema Marekani "imejiondoa kutoka kwa kuwa mhusika mkuu katika shughuli ya kutafuta amani".
      Hadhi ya mji wa Jerusalem imekuwa sehemu ya mzozo wa Waisraeli na Wapalestina.
      Kwa nini Jerusalem inazozaniwa?
      Mji huo una maeneo matakatifu ya dini tatu zenye kufuata imani ya Ibrahim - Uyahudi, Ukristo na Uislamu - sana maeneo mengi yanapatikana Jerusalem Mashariki.
      Israel ilitwaa eneo hilo kutoka Jordan wakati wa vita kati ya nchi za Kiarabu na Israel mwaka 1967 na imekuwa ikiuchukulia mji wote kuwa mji wake mkuu ambao hauwezi kugawanywa.
      Jerusalem Mashariki hutazamwa kuwa mji mkuu wa taifa la Wapalestina (litakapoundwa) na mataifa ya Kiarabu na Kiislamu pamoja na Wapalestina wenyewe.
      Kwa mujibu wa maafikiano wakati wa mazungumzo ya amani ya Wapalestina na Waisraeli ya 1993, hatima ya mji huo ilifaa kuamuliwa wakati wa hatua za mwisho za mazungumzo.
      Jerusalem
          Hatua ya Israel kudhibiti Jerusalem yote haijawahi kutambuliwa kimataifa na nchi zote zina afisi za kibalozi Tel Aviv.
          Tangu 1967, Israel imejenga makazi kadha ya Wayahudi na kuna takriban walowezi 200,000 wa Kiyahudi eneo hilo. Makazi haya yamekuwa yakishutumiwa na jamii ya kimataifa.
          Kwa nini Trump akafanya hivyo ?
          Rais Trump alisema kwamba "ameamua ni wakati mwafaka kutambua rasmi Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel."
          "Nimeamua hatua hii itakuwa ndiyo bora zaidi kwa maslahi ya Marekani katika juhudi za kutafuta amani kati ya Waisraeli na Wapalestina," alisema.
          Alisema ameiagiza wizara ya mambo ya nje ya Marekani kuanza kuuhamisha ubalozi wa Marekani kutoka Tel Aviv hadi Jerusalem.
          Licha ya onyo kwamba hatua kama hiyo inaweza kuzua wimbi la machafuko kanda ya Mashariki ya Kati, hatua hiyo inatimiza ahadi aliyoitoa Trump wakati wa kampeni na pia kuwafurahisha wafuasi wenye msimamo mkali wa Bw Trump.
          Jerusalem
          Bw Trump alisema kutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel ilikuwa "ni kutambua uhalisia tu," na akaongeza kwamba "ndiyo hatua ya busara kuichukua."
          Bw Trump alisema Marekani itaendelea kuunga mkono suluhu ya mataifa mawili - taifa la Waisraeli na Wapalestina - mataifa yote yakiishi pamoja kwa amani.
            Rais huyo pia alijizuia kurejelea msimamo wa Israel kwamba Jerusalem ni mji wake mkuu wa milele ambao hauwezi kugawanywa.
            Wapalestina wanataka Jerusalem Mashariki iwe mji mkuu wa taifa la Wapalestina litakapoundwa

            Maoni

            Machapisho maarufu kutoka blogu hii

            MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

            Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

            Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

            MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

            Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

            Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...