Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mabondia wanne watambuliwa na rais Kenya

MTEULE THE BEST

Fatuma Zarika akikabiliana na Belinda Laracuente wa Puerto Rico katika pigano la kutetea ubingwa wa dunia upande wa wanawake uzani wa feather.
Fatuma Zarika (kushoto) akikabiliana na Belinda Laracuente wa Puerto Rico awali
Bingwa wa dunia uzani wa super-bantam chama cha WBC Fatuma Zarika na Rayton Okwiri ni miongoni mwa mabondia wanne wa Kenya wa kulipwa ambao Jumanne wiki hii wamepata tuzo ya heshima kutoka kwa Rais Uhuru Kenyatta kuadhimisha siku kuu ya Jamhuri.
Mabondia hao wanne wamepata tuzo inayojulikana kama Head of State Commendation (HSC).
Mbali na Zarika na Okwiri, wengine waliopata tuzo hiyo ni Maurice Okolla na James Onyango ambaye hivi majuzi alishinda taji la World Boxing Organisation (WBO) uzani wa welter kwa kumshinda Saidi Mundi wa Tanzania katika hoteli ya Carnivore jijini Nairobi.
Wakati Onyango akimshinda Mundi, Zarika naye siku hiyo hiyo alihifadhi taji lake la dunia kwa kumshinda kwa pointi Catherine Phiri wa Zambia katika pigano la raundi kumi uzani wa super-bantam, naye Okwiri akamshinda kwa pointi bondia mwingine wa Tanzania Imani Daudi.
Zarika, mwenye umri wa miaka 32, alitwaa mkanda huo mwaka jana huko Michigan, Marekani, kwa kumshinda kwa pointi Alicia Ashley wa Jamaica. Hii ilikua ni mara ya kwanza anatetea ubingwa wake wa dunia dhidi ya Phiri.
Kwa matokeo hayo Zarika ameshinda mapigano 30, akapoteza mara 12 na kwenda sare mara mbili.
Zarika akiwa na bondia mstaafu Mike Tyson nchini Marekani
Zarika akiwa na bondia mstaafu Mike Tyson nchini Marekani
Miongoni mwa mapigano hayo 30 aliyoshinda, 17 ni kwa knockout.
Zarika alijiunga na ndondi mwaka wa 2000 mtaa wa Mathare jijini Nairobi, akashinda mapigano matatu na akapoteza mara moja katika ndondi za ridhaa. Laila Ali, bintiye bondia mashuhuri duniani Muhammad Ali, ndiye alichangia sana Zarika kujifunza ndondi.
"Nilivutiwa sana na vile alikua anacheza nilipomtizama kwenye TV nami nikaamua nataka niwe kama Laila,'' anasema Zarika.
Mwaka wa 2011 aliamua kucheza ndondi za kulipwa, na miongoni mwa mabondia alioshinda hapo mwanzo ni Rukken Koronoso wa Afrika Kusini na Esther Herkole

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...