Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mourinho: Ningekuwa likizoni Brazil au Los Angeles

MTEULE THE BEST

Meneja wa klabu ya Manchester United Jose Mourinho amesema "angelikuwa likizoni Brazil au Los Angeles" iwapo angekuwa anaamini kwamba mbio za Ligi ya Premia msimu huu zimepata mshindi.

Alisema hayo baada ya klabu yake kulaza Bournemouth 1-0 Jumatano.

United walijikwamua kutoka wka kichapo cha Manchester City wikendi lakini hawakuweza kupunguza mwanya kati yao na City ambao wamo alama 11 mbele yao kwani vijana hao wa Etihad walilaza Swansea 4-0.

Romelu Lukaku ndiye aliyewafungia Man United bao hilo la ushindi kipindi cha kwanza.

Mourinho alisema: "Mechi hiyo dhidi ya City ilikuwa kubwa, na ukishindwa hilo halisaidii juhudi zako za kujiweka sawa tena - ushindi husaidia, kushindwa hakusaidii.

"Bournemouth walikuwa wapinzani wakali na hali ilikuwa ngumu. Kama tungelifunga bao la pili tungetulia.

"Nimefurahishwa na alama hizo tatu. Walipumzika siku moja zaidi yetu, walikuwa sawa kutushinda baada ya kupumzika, hata kiakili kwa sababu mechi kubwa huwadhoofisha wachezaji zaidi.

"[Mbio za ligi] zitamalizika tu Mei. Kama zingekuwa zimemalizika sasa ningeenda likizo Brazil au Los Angeles."

Msimamo wa Mourinho ni tofauti na meneja wa Chelsea Antonio Conte ambaye amekiri kwamba itakuwa vigumu kuwazuia Manchester City.


Beki wa Manchester United Luke Shaw alianza mechi kwa mara ya kwanza ligini msimu huu

United walikuwa wamecheza mechi 40 nyumbani bila kushindwa hadi walipolazwa na vijana hao wa Pep Guardiola Jumapili.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...