Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Trump aidhinisha Marekani kutuma watu tena kwenye Mwezi

MTEULE THE BEST

U.S. President Donald Trump holds up "Space Policy Directive 1" after signing it during a ceremony.
Rais wa Marekani Donald Trump ameliagiza shirika la anga za juu la Marekani kupanga tena kutuma binadamu kwenye Mwezi kwa mara ya kwanza tangu 1972.
Mpango huo utaangazia upelelezi wa muda mrefu pamoja na uwezekano wa kutumiwa kwa uso wa Mwezi, kwa ushirikiano na sekta ya kibinafsi.
Bw Trump amesema mpango huo utaweka msingi wa kuwezesha mwishowe kutuma watu sayari ya Mars, ingawa hakutoa tarehe ya ni lini hilo linapangiwa kufanyika.
Wachanganuzi wanasema juhudi zozote kama hizo zitahitaji Bunge la Congress kukubali kuongezea shirika hilo fedha zaidi.
      Wabunge Marekani huunga mkono upelelezi zaidi anga za juu lakini hutofautiana kuhusu malengo na bajeti.
      Mapema mwaka huu, China ilitangaza kwamba inajiandaa kutuma binadamu kwenye Mwezi kwa mara ya kwanza.
      Bw Trump, akiidhinisha mpango huo wake mpya, alisema: "Sisi ndio tunaoongoza na tutaendelea kusalia kuwa viongozi, na tutaongeza hilo sana."
      This NASA file photo taken on July 20, 1969 shows astronaut Edwin E. "Buzz" Aldrin, Jr. saluting the US flag on the surface of the Moon
      Mpango huo wa sasa unatarajiwa kuweka msingi wa kuwezesha mwishowe kutuma watu sayari ya Mars
      Hatua ya Bw Trump ilipendekezwa na Baraza la Taifa la Anga za Juu ambalo huongozwa na makamu wa rais Mike Pence.
        Agizo la Trump limeenda kinyume na mpango uliowekwa na mtangulzii wake Barack Obama, wa kuangazia zaidi kutuma binadamu katika sayari iliyo karibu na dunia

        Maoni

        Machapisho maarufu kutoka blogu hii

        MAPENZI: Kuna faida na ni muhimu Mpenzi wako kuwa rafiki yako pia

        Kuna faida kubwa kwa wapenzi kuwa marafiki KUTOKANA na mila mbalimbali, baadhi ya watu wamekuwa wakiamini kwamba mwanamke ni daraja la pili. Daraja la kwanza na lenye kuthaminiwa ni mwanaume. Yaani mwanamke hana kauli kwa mwanaume. Anakuwa kama mtumwa fulani hivi.  Mwanaume akiongea, basi ni maelekezo kama vile rais wa nchi anavyotoa maelekezo kwa watu walio chini yake. Hakuna wa kupinga. Akisema sitaki kitu fulani kifanyike, basi ni mpaka atakapotoa maelekezo mengine. Vinginevyo, maelekezo ya awali yatabaki kusimama kama sheria.  Wapo baadhi ya wanawake wanaofurahia aina hii ya uhusiano kwa sababu ya mazoea. Kwamba wamekuzwa hivyo, mwanaume ni mwanaume. Huu ni mfumo ambao watu wengi wamekuwa wakiuishi. Kuna ambao wanakubaliana nao, wengine hawakubaliani nao.  Watu wengi sana wamekuwa wakiishi katika malumbano katika mahusiano yao kutokana na mfumo huu wa maisha. Mwanamke hataki kuishi kama mtumwa, mume anakomaa kuonesha uanaume wake. Hakuna anayekubali kushuka,...

        Urusi: Vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini havitafua dafu

        MTEULE THE BEST Image caption Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov na mwenzeka wa Marekani Rex Tillerson Waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Segei Lavrov amemwambia waziri wa ulinzi nchini Marekani Rex Tillerson kwamba kuiwekea vikwazo zaidi Korea Kaskazini hakutafua dafu. Taarifa iliochapishwa na wizara ya kigeni nchini Urusi inasema kuwa wawili hao walizungumza kwa njia ya simu na kushutumu majaribio ya makombora ya hivi karibuni yaliotekelezwa na Pyongyang . Lakini inasema kuwa bwana Lavrov alisisitiza kwamba diplomasia ndio njia ya pekee ya kumaliza wasiwasi katika rasi ya Korea, na kutaka hatua zozote dhidi ya taifa hilo kusitishwa akionya huenda zikasababisha madhara yasiojulikana. Waziri wa ulinzi nchini Marekani amesisitiza kuwa bado kuna fursa ya kidiplomasia katika kukabiliana na Korea Kaskazini. Mapema rais Trump alichapisha ujumbe katika akaunti yake ya Twitter akisema mazungumzo sio suluhisho.

        Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania

        Fuvu la binadamu wa kale liligunduliwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania Miaka 60 siku kama ya leo ugunduzi mkubwa ulifanyika katika eneo la Olduvai Gorge, kwenye kreta ya Ngorongoro. Wanaakiolojia Louis na Mary Leakey waligundua fuvu la mtu anayeaminika kuwa ni wa kale zaidi waliyompa jina la Zinjanthropus. Ugunduzi huo uliofanyika saa nne asubuhi Julai 22, 1959 kipindi hicho kwenye eneo la Tanganyika ulikuwa wa vipande zaidi ya 100 ukasaidia katika kutambua asili ya watu wa awali duniani. Kabla ya ugunduzi huo, wanasayansi na wanahistoria walikuwa wakiamini kuwa binadamu wa kale walitokea Uchina baada ya ugunduzi wa mafuvu ya kale baina ya 1923 na 1927 nchini humo ya Homo eractus, ama maarufu kama Peking Man. Mafuvu hayo ya Uchina yalikuwa na umri wa takribani miaka 750,000. Mafuvu ya Olduvai eneo ambalo kwa sasa lipo Tanzania wakati wa ugunduzi wake lilikuwa na umri wa takribani miaka milioni 1.75, na hakuna mabaki ya mtu wa kale zaidi ambayo mpaka sasa yamegundul...